Tuesday, July 21, 2009

Tuwe makini na hawa wanyama

Haya chacha na yeye kachukia angalia kivumbi chake sijui utambambia nini atulie mtu chali, watu mbio mh! we have to be carefully

Friday, July 10, 2009

ENJOY YOUR WEEKEND

Jamani nawatakia weekend njema najua mambo ya full shangwe ni kawaida ndo maana nimewawekea Remix ya full shangwe ya HUssein machozi tuburudike kabla ya kutembelea sehemu za starehe kwanza.

Enjoy your weekend.

Thursday, July 9, 2009

Msichana mfupi kuliko wote Duniani

Jyoti akiwa na marafiki zake wa shule.
Jyoti akiwa masomoni darasani.


Joyti akiwa na mtoto wa ndugu yake wa umri wa mwaka mmoja.

JOyti akiwa anajisomea




JOyti akiwa darasani

Joyti akiwa amebebwa na wazazi wake.
anaitwa joyti jamani siyo joti, Jyoti Amge wa nchini India ndiye msichana mfupi kuliko wote duniani pamoja na kuwa na umri wa miaka 15 ana urefu wa sentimeta 38 tu na tangia amezaliwa ameongezeka kilo nne tu na kutokana na ufupi wake hata mtoto wa mwaka mmoja anaonekana mkubwa zaidi yake. habari zaidi unaweza ukatembelea

Wednesday, July 8, 2009

Mfalme mpya wa tenisi duniani

Mchumba wa Roger Federer, Miroslava Vavrinec(wa mbele) na mke wa Roddick, Brooklyn Decker wakishuhudia sweet hearts wao wakipambana.
Ni mpambano wa fainali za Wimbledon 2009, Roger Federer Vs Andy Roddick

Federer na mpinzani wake, Andy Roddick


Federer, we acha tu



Aliyekuwa mfalme wa tenisi duniani, Peter Sampras akitoa alama ya kukabidhi ufalme kwa Roger federer baada ya fainali za Wimbledon.




Mfalme mpya wa Tenisi duniani, Roger Federer akibusu kombe.







Federer akishangilia ushindi dhidi ya Roddick
Federer ametwaa kombe la Wimbledon kwa mara ya SITA, na ni mara ya 15 anatwaa makombe makubwa ya tenisi.
Sampras ametwa mataji saba ya Wimbledon, na 14 ya kimataifa.




Siku ya kumuaga mfalme wa pop duniani

Familia ya Michael Jackson kwenye shughuli ya jana
haya chacha mama na t-shirt

Dada wa Michael Jackson,Janet na Latoya wakimfariji mtoto wa Michael, Paris



Jeneza lenye mwili wa Michael Jackson linalo sadikiwa kugharimu dola 25,000 za kimarekani


Kaka wa Michael, Marlon akizungumza kwenye shughuli ya jana, uchungu ulisababisha ashindwe kuendelea.




Enzi za uhai wa king wako jacko.













picha juu king of pop akiwa na watoto wake enzi za uhai wake.






Mtoto wa kwanza wa Michael, Prince akiwa na dada yake, Paris katika shughuli ya kumuaga baba yao jana jijini Los Angeles.








Michael Jackson enzi hizo.









Ndugu wa Michael wakimfariji Paris baada ya mtoto huyo kuwatangazia mamilioni ya watu kote duniani upekee wa baba yake na namna anavyompenda.
Kauli ya mtoto huyo ilisababisha watu wengi wabubujikwe machozi, dah inatia uchungu.











Ndugu wa Michael wakiwamo wasanii wa The Jackson Five wakibeba jeneza lenye mwili wa Michael Jackson jana.










Wanamlilia Michael












Umati uliofika ukumbini jana jijini Los Angeles kumuaga Michael. Watu 20,000 walikuwa ukumbini humo.

SIJAWAHI kushuhudia mtu akiagwa kama Michael Jackson na sidhani kama nitaweza kuona tena hali kama hiyo katika siku za uhai wangu.
Kwa ambaye hakuwa anafahamu nafasi ya Michael katika jamii, yaliyotokea na kusemwa jana yalitosha kumfahamisha hilo, Michael was SPECIAL na hakuna wa kumfananisha naye.
Michael ameaga dunia lakini muziki wake na maisha yake kwa ujumla vitasababisha aendelee kuishi leo na kizazi kijacho.
Dunia imewahi kuwa na wanamuziki wengi, lakini haijawahi kuwa na mtu mwenye karama kama Michael Jackson, anayebisha hajui asemalo.
Alikuwa mwanadamu kama mimi na wewe, alikuwa na udhaifu kama tulionao mimi na wewe, lakini kamwe hatuwezi kujilinganisha naye, he was the biggest star on earth!
Alikuwa na nguvu, si tu za kifedha au kisanii, alikuwa na mvuto wa kipekee kulinganisha wanamuziki wote unaowafahamu.
Michael was the greatest ENTERTAINER on earth, Michael was the greatest STAR earth, kwa wanawe, Michael was the GREATEST father ever!
Buriani Michael, pumzika kwa amani, Amen.












Jinsi mtoto wa Wako Jacko alivyo sababisha simanzi

Paris akizungumza wakati wa shughuli ya kumuenzi baba yake jana jijini Los Angeles,Marekani


Baada ya kueleza anavyompenda baba yake, Paris alishindwa kuvumilia, alianza kulia na kusababisha simanzi ukumbini na popote walipokuwa wakitazama tukio hilo la kihistoria.



Dada na Michael, Janet, akimkumbatia Paris kumfariji.
LILIKUWA tukio la nadra, halikutarajiwa, na ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mtoto wa Michael Jackson kuzungumza hadharani tena mbele ya umati wa watu.
Watoto wa Mfalme huyo wa muziki wa Pop wamekuwa wakiishi maisha ya usiri ikiwa ni pamoja na kuficha sura zao kwa mask.
Jana ilikuwa ni mara ya pili kwa watoto hao, Prince, Paris na Prince II kuonekana hadharani bila kuficha sura zao.
Kwa mara ya kwanza walionekana hivyo Mei mwaka huu wakiwa mtaani na baba yao wakati wakienda studio.
Aliyoyasema Paris Jana ndiyo taarifa kubwa kwenye vyombo vya habari vya kimataifa hivi sasa, maneno yake yamegusa wengi nikiwamo mimi.
Alisema hivi:
"Ever since I was born, Daddy has been the best father I could imagine,"
Baada ya kutamka maneno hayo alianza kububujikwa machozi, akamuegemea shangazi yake, Janet, na akajitahidi kuzungumza tena akasema:
"I just want to say I love him so much."
Mtoto huyo aliyasema hayo akiwa jirani na jeneza la marehemuMichael Jackson.


Friday, July 3, 2009

Taswira


Pichani ni Taswira ya huko kwa wenzetu sasa ni lini na bongo itakuwa hivyo? kunamdau aliniambie eti mpaka mwaka 21099 du!!!!!!!!!!!!!!!!! ni kweli hayo Viongozi wamaendeleo ya nchi wakiamua si tutafika hapo

Thursday, July 2, 2009

Haya sasa 77 kumekucha

Kama picha inavyo onesha bendera za nchi mbalimbali zikipepea
Na hapa ndiyo sehemu ya kuingilia ndani

Wednesday, July 1, 2009

Du! Nimeshindwa kutambua

Hiki ni kichina,kiswahili au ni kiinglishi maana mh!

TAMASHA LA ZIFF ZANZIBAR

Amani Enssemble kutoka bara wakifanya vitu vyao



Pichani ChiniSwahili Vibes wakatoa mambo ya Pwani.


Na hawa ni karafuu Band








NDEGE AINA YA YEMENIA YAANGUKA COMORO

Ndege ya Yemen yaanguka Comoro
Ndege ya abiria ya Yemeni ikiwa na watu zaidi ya 150 imeanguka katika bahari ya Hindi karibu na visiwa vya Comoro.
Baadhi ya miili imepatikana na waliosalimika kuokolewa, maafisa kutoka shirika la ndege hiyo, Yemenia, wameeleza.
Ndege hiyo muundo wa Airbus 310 ikiwa na safari namba IY626 ilikuwa ikisafiri kutoka Sanaa mji mkuu wa Yemen, lakini idadi kubwa ya abiria walianzia safari yao Ufaransa.
Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana. Waziri mmoja wa Ufaransa amesema hitilafu kadhaa ziligundulika wakati ndege hiyo ilipokaguliwa maswala ya kiufundi mwaka 2007.
"Ndege aina ya A310 iliyohusika ilikaguliwa mwaka 2007 na mamlaka ya usafiri ya Ufaransa (DGAC) na waligundua hitilafu kadhaa. Tangu wakati huo ndege haijawahi kurejea Ufaransa," Waziri wa Usafirishaji wa Ufaransa, Dominique Bussereau alinukuliwa akiieleza televisheni moja ya Ufaransa.
"Kampuni hiyo haikuwa katika orodha ya makampuni yaliyopigwa marufuku lakini ilikuwa chini ya uangalizi wa masharti magumu ya ukaguzi, na ilikuwa ikitarajiwa kuhojiwa na kamati ya maswala ya usalama ya Umoja wa Ulaya."
Awali Bw Bussereau alivieleza vyombo vya habari vya Ufaransa kuwa hali mbaya ya hewa huenda ilisababisha ajali hiyo.
Ramani inayoonyesha njia ilikopita ndege hiyo.
Taarifa zinaeleza kuwa ndege hiyo ilikuwa ikitarajiwa kutua Moroni mji mkuu wa Comoro majira ya saa nane na nusu. Abiria wengi kati yao walisafiri kwenda Sanaa wakitokea Paris na Marseille kwa kutumia ndege tofauti.
Ndege hiyo waliyounganisha kwenda Moroni inasemekana ilisimama kwa muda nchini Djibouti.
Kulikuwa na watu zaidi ya 150 ndani yake wakiwemo watoto wachanga watatu na wafanyakazi 11.Habari katika picha