



Jeneza lenye mwili wa Michael Jackson linalo sadikiwa kugharimu dola 25,000 za kimarekani




picha juu king of pop akiwa na watoto wake enzi za uhai wake.



Kauli ya mtoto huyo ilisababisha watu wengi wabubujikwe machozi, dah inatia uchungu.

Ndugu wa Michael wakiwamo wasanii wa The Jackson Five wakibeba jeneza lenye mwili wa Michael Jackson jana.


SIJAWAHI kushuhudia mtu akiagwa kama Michael Jackson na sidhani kama nitaweza kuona tena hali kama hiyo katika siku za uhai wangu.
Kwa ambaye hakuwa anafahamu nafasi ya Michael katika jamii, yaliyotokea na kusemwa jana yalitosha kumfahamisha hilo, Michael was SPECIAL na hakuna wa kumfananisha naye.
Michael ameaga dunia lakini muziki wake na maisha yake kwa ujumla vitasababisha aendelee kuishi leo na kizazi kijacho.
Dunia imewahi kuwa na wanamuziki wengi, lakini haijawahi kuwa na mtu mwenye karama kama Michael Jackson, anayebisha hajui asemalo.
Alikuwa mwanadamu kama mimi na wewe, alikuwa na udhaifu kama tulionao mimi na wewe, lakini kamwe hatuwezi kujilinganisha naye, he was the biggest star on earth!
Alikuwa na nguvu, si tu za kifedha au kisanii, alikuwa na mvuto wa kipekee kulinganisha wanamuziki wote unaowafahamu.
Michael was the greatest ENTERTAINER on earth, Michael was the greatest STAR earth, kwa wanawe, Michael was the GREATEST father ever!
Buriani Michael, pumzika kwa amani, Amen.
No comments:
Post a Comment